Walimu wajengewa choo Mirerani, wanafunzi wapewa chakula na sare za shule

Diwani wa Kata ya Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Salome Mnyawi (kulia) akikabidhi moja kati ya magunia matatu ya chakula kwa wanafunzi wa shule ya msingi Songambele ili wale chakula shuleni. Picha na Joseph Lyimo

Mirerani. Changamoto ya walimu wa shule ya msingi Songambele wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara kujisaidia choo kimoja na wanafunzi imepatiwa ufumbuzi baada ya diwani wa Mirerani, Salome Mnyawi kuwajengea choo.

Mnyawi wakati akikabidhi choo hicho leo Alhamisi Machi 4, 2021 amesema pia amenunua magunia ya mahindi na maharage ili wanafunzi hao wale chakula shuleni.

"Nimetimiza ahadi yangu ya kuwajengea walimu choo kwa gharama zangu, nikawanunulia chakula magunia mawili ya mahindi na moja la maharage kisha mdau wangu Rachel Njau akawanunulia wanafunzi yatima 24 sare za shule," amesema Mnyawi.

Njau ambaye ni katibu wa chama cha wachimbaji madini mkoani Manyara (Marema) tawi la Mirerani amesema baada ya Mnyawi kumweleza changamoto ya sare za wanafunzi hao alinunua mashati, sketi, kaptula, nguo za ndani na soksi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments