Tusihofu: Bado mbili za mwisho

Tusubiri mechi mbili za mwisho

IMEBAKI michezo miwili kufahamu mustakabali wa Tanzania katika kundi F, baada ya leo kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Morocco.

Katika mchezo huo uliopigwa muda mchache uliopita uwanja wa Laurent Pokou San Pedro, Stars imepoteza mabao 3-0.

ISOME NA HII >TFF: Kauli Za Amrouche Hatuzitambui

Mabao ya Morocco yamefungwa na Roman Saiss, Azzedine Ounahi na Youssef En-Nesyri.

Stars sasa itasubiri mchezo unaofuata dhidi ya Zambia utakaochezwa Januari 21, 2024 katika uwanja huo.

Mchezo wa mwisho wa kumaliza hatua ya makundi, Tanzania itakutana na DR Congo Januari 24.

Ili kufufua matumaini ya kusonga 16 bora, Stars inapaswa kushinda mchezo unaofuata dhidi ya zambia.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments