Kocha huyo amesema
nafasi ambazo wamezilenga kwenye usajili huo ni viungo wawili pamoja na
mshambuliaji mmoja.
ISOME NA HII - VIDEO: Ladack Chasambi hapoi ameanza Mazoezi Mepesi Visiwani Zanzibar
“Lengo letu ni
kuongeza wachezaji wasiozidi watatu kwenye dirisha dogo, tunajua siyo kazi
rahisi kupata mchezaji mwenye ubora kipindi hiki lakini tutaangalia
tukifanikiwa itakuwa vizuri na kama tutakosa siyo mbaya sababu tuna wachezaji
wengi kwenye kikosi chetu,” - amesema Chamberi.
Aidha, kocha huyo
ambaye ameachiwa mikoba ya Mecky Maxime aliyefutwa kazi wiki tatu zilizopita,
amesema timu hiyo tayari imeanza mazoezi kwa ajili ya kumalizia mechi mbili
zilizobaki kwenye mzunguko wa kwanza Ligi Kuu Tanzania Bara.
Amesema anajua timu
hiyo haipo nafasi nzuri na wana mlolongo mbaya wa matokeo na atakachokifanya
yeye na wasaidizi wake ni kuimarisha sehemu zenye mapungufu, ili kufanya vizuri
na kubadili mwenendo wa timu hiyo.
Kagera Sugar ipo nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu, ikikusanya alama 13 katika idadi kama hiyo ya mechi walizocheza.
#SINGIDA: Taarifa Kwa UMMA kutoka SIREFA #BandolaMedia pic.twitter.com/hjf1u8BtxX
— Bandola Media (@bandolamediatz) January 9, 2024
0 Comments