
Baada ya kupendekezwa, jina la mwanachama huyo litapelekwa haraka kwa Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kwa ajili ya uteuzi wa nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, akichukua nafasi ya Maalim Seif aliyefariki dunia Februari 17 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matitabu.
Kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, kamati ya uongozi inaundwa wajumbe tisa ambao ni viongozi wakuu wa chama hicho kati yao wawili hawapo ambao, ni Maalim Seif huku Bernard Membe akijiuzulu nafasi hiyo, baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
0 Comments