Kumekucha ACT-Wazalendo


Dar es Salaam. Kamati ya Uongozi ya Chama cha ACT-Wazalendo, inatarajiwa kukaa muda wowote kuanzia leo kwa ajili ya kuchambua na kupendekeza jina la mwanachama atakayemrithi Maalim Seif Sharif Hamad katika nafasi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar.

Baada ya kupendekezwa, jina la mwanachama huyo litapelekwa haraka kwa Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kwa ajili ya uteuzi wa nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, akichukua nafasi ya Maalim Seif aliyefariki dunia Februari 17 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matitabu.

Kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, kamati ya uongozi inaundwa wajumbe tisa ambao ni viongozi wakuu wa chama hicho kati yao wawili hawapo ambao, ni Maalim Seif huku Bernard Membe akijiuzulu nafasi hiyo, baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments