Viongozi ‘wababe’ waonywa, watakiwa kuzingatia taratibu za utumishi

 

Mtwara. Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi amewataka viongozi wa umma kuwa na akiba ya maneno hasa wanapoona vyombo vya habari.

Akizungumza na watumishi wa Mkoa wa Mtwara amesema imekuwa kawaida viongozi kutoa kauli zinazowaingiza kwenye migogoro na watumishi wenzao  hali aliyosema inapoteza dhana ya utawala bora.

Amebainisha kuwa katika kipindi hiki hatarajii kuona migogoro kazini wala viongozi kuwaweka ndani watumishi na kutaka mtumishi aadhibiwe kulingana na taratibu za utumishi ikiwemo kumwagiza mkurugenzi kumuandikia barua ya onyo.

watumishinyinginepic

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Deogratius Ndejembi (wapili kushoto) akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Dunstan Kyobya wakitembelea baadhi ya Kaya masikini manispaa ya Mtwara Mikindani.

"Wapo wenye mamlaka ya kuweka watumishi ndani haya ni matumizi mabaya ya madaraka,  hivi tukiamua kuwawajibisha kwa kufuata taratibu za  utumishi hamuoni itasaidia sana kuliko kuwaweka ndani, jaribuni kujishusha.”

"Chukueni hatua kwa watumishi ambao wamehatarisha amani na usalama wa nchi na mtumishi akikosea asionewe hatua zichukuliwe stahiki. Mfano akutwe anafanya biashara za magendo huyo mchukulieni hatua haraka lakini kwa makosa mengine hatua za utumishi  zifuatwe, ila sio umemkuta kwenye starehe usiku, asubuhi unamchukulia hatua, huu si utawala bora,” amesema.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments