Rais Samia ametoa maelekezo hayo wilayani Uyui mkoani Tabora wakati akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo, katika ziara yake ya mkoa huo iliyokwenda sambamba na ufunguzi wa barabara ya Nyahua –Chanya- Uyui-Tabora.
Katika maelezo yake, Rais Samia amesema kuna zabuni za ununuzi wa vifaa vya afya bado zinasuasua kwenye mamlaka za Serikali za Mitaa,akimtaka Bashungwa kusimamia vyema eneo hilo.
"Mwisho wa matumizi ya fedha za Uviko-19 Juni mwaka huu, na kwamba fedha zote zinahitajika kutumiwa kwa wakati ili kukidhi vigezo vya kupata nyingine zaidi. Waziri ahakikisha memuagiza Waziri Bashungwa Zabuni zinafanyiwa kazi kwa wakati ili kazi hizo zikamilike kwa wakati.
“Ucheleweshaji wa zabuni hizo utasababisha fedha nyingi kutotumika kwa wakati na kusababisha ukiukwaji wa malengo ya fedha hizo, suala hilo litasababisha fedha kurudishwa na kukosa fedha nyingine za maendeleo.Nakuagiza waziri wa Tamisemi kasimamie hili” amesema Rais Samia
Kuhusu matumizi ya fedha kwenye halmashauri Rais Samia ameziagiza halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatumia fedha zinazotolewa na Serikali kwa kazi zilizokusudiwa za kutatua kero za wananchi
Rais Samia amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwenye ngazi ya Halmashauri lengo likiwa ni kutatua kero za wananchi katika sekta ya afya, elimu, maji hivyo zisimamie na kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na Serikali.
0 Comments